India: Majiko yaliyoboreshwa yaondolea adha wanawake kuvaa miwani wakipika
MP3•منزل الحلقة
Manage episode 425393951 series 2027789
المحتوى المقدم من UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. يتم تحميل جميع محتويات البودكاست بما في ذلك الحلقات والرسومات وأوصاف البودكاست وتقديمها مباشرة بواسطة UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations أو شريك منصة البودكاست الخاص بهم. إذا كنت تعتقد أن شخصًا ما يستخدم عملك المحمي بحقوق الطبع والنشر دون إذنك، فيمكنك اتباع العملية الموضحة هنا https://ar.player.fm/legal.
Katikati ya bonde la mto Ganges kaskazini mwa India, ndiko liko jimbo la Bihar ambalo sasa linahaha kutokana na uchafuzi wa hewa, kwani moshi utokao kwenye majiko ya kuni na samadi ya ng’ombe yanasababisha kwa kiasi kikubwa uchafuzi wa hewa. Licha ya maendeleo makubwa ya kutumia gesi kama chanzo cha nishati, halikadhalika nishati itokanayo na samadi, bado familia au kaya maskini zinashindwa kumudu vyanzo hivyo na kujikuta vikutumia kuni au samadi ya ng’ombe kupikia, ambavyo huchafua hewa. Sasa Benki ya Dunia imewezesha kuundwa kwa vikundi vya kujiwezesha au SHGs ambapo wanawake wanapatiwa elimu ya masuala mbali mbali ikiwemo nishati salama na hivyo kuboresha afya zao. Assumpta Massoi kupitia video ya Benki ya Dunia amefuatilia mradi huo na kuandaa makala hii.
…
continue reading
100 حلقات